Monday, July 22, 2013

Chapati

Wadau Asalaam Aleykum kwa Waislam wote na Bwana Asifiwe kwa Wakristu wote.
Leo dada yenu naja na pishi la CHAPATI. Najua ni kitafundwa pendwa sana na kinapendwa na kila lika.
Uzuri wake chapati bwana unaweza kulia na chochote kile, iwe maharage, supu aina zote, mchuzi uwe wa kuku, wa samaki, wa nyama yani raha tupu hapa hata na chai inapanda kwa soda na juice tena ndio balaaa.
Kwa kipindi hiki cha mfungo mtukufu wa Ramadan chapati hua zinalika hasa tena sana sana hua zinaambatana na mchuzi no matter wa kitoweleo gani.
Tuungane pamoja katika safu yetu na tushare pamoja mawazo yetu.
 
 
Mahitaji
ü  Unga wa ngano (Plain flour 1kilo)
ü  Siagi (Butter vijiko 2 vya chakula)
ü  Yai (Egg 1)
ü  Chumvi (1/2 ya kijiko cha chai)
ü  Hiliki (Ground cardamon 1/4 ya kijiko cha chai)
ü  Maji ya uvuguvugu (Warm water)
ü  Mafuta ya kupikia (Vegetable oil)
 
Matayarisho
Weka unga wa ngano katika bakuli la kukandia, kisha tia chumvi na  hiliki iliyo twangwa na uchanganye kwanza mpaka mchanganyiko wako uchanganyike.
Tia siagi na uichanganye vizuri na unga mpaka ipotee. Baada ya hapo tia tena yai na uchanganye vizuri.
Mchanganyiko ukishachanganyika vizuri sasa unaweza kutia maji ya uvuguvugu kidogo, kidogo huku ukiwa unauchanganya ili kupata donge.

Baada ya hapo anza kukanda hilo donge mpaka mabuje yote yapotee na unga uwe laini.
ambapo itakuchukua kama dakika kumi au kumi na tano hivi. Baada ya hapo kata kata unga wako katika madonge ya wastani yani si makubwa si madogo.
Baada ya hapo andaa kibao cha kusukumia chapati kwa kukitia unga kidogo ili chapati isinatie kwenye kibao.
Sukuma donge moja la chapati mpaka liwe flat na kisha weka kijiko kimoja cha mafuta na usambaze.
Ukisha maliza ikunje (roll). Ufanye hivyo na kwa madonge yote yalio bakia.
Baada ya hapo andaa chuma cha kuchomea (fry-pan) katika moto wa wastani.
Kisha anza kusukuma chapati (ni vizuri ukaanza na zile ulizozikunja mwanzo ili kuzipa nafasi zile za mwisho ziweze kulainika).
Ukiwa unasukuma hakikisha zinakuwa flat (na zisiwe nene sana au nyembamba sana) Ukishamaliza hapo tia kwenye chuma cha kuchomea.
Acha iive upande mmoja kwanza alafu uigeuze na  upande wa pili.
Tia mafuta ama kijiko kimoja kikubwa upande wa chini wa chapati na uanze kuukandamiza kwa juu uku ukiwa unaizungusha.
Utaendelea kufanya hivyo uku ukiwa unaigeuza kuiangalia kwa chini ili isiungue. ikishakuwa ya brown, geuza upande wa pili na urudie hivyo hiyvo mpaka chapati iive.
Utaitoa na kuiweka kwenye sahani na itakua tayari kwa kuliwa.

Utafanya hivyo kwa madonge yako ya chapati yote yaliyo bakia.

Swaum Njema na Ramadan Kareem.

Tuesday, July 16, 2013

Take It or Leave It

Facts of Life
Important
May Allah forgive us our sins and  accept our prayers, bless us with his love and care, throught out life and hereafter.

Wishing you a wonderful Ramadan.

Friday, July 12, 2013

Hijab styles

It’s all about swagzzz…. Hahahaha ona swag za hijab hadi za watoto
 

 Open hii link ku-enjoy zaidi 
 
Swaum njema.
Ramadan Maqbul & Jumaa Mubarak

Thursday, July 11, 2013

Ramadan Kareem

It’s officially RAMADAN Alhamdulillah.
 
May Allah keep us steadfast on the Deen and may he make this month a means to grant us Jannah.
 
Note: When the month RAMADAN start the gates of the heaven are opened and the gates of hell are closed, also the devils are chained.
 
 
 
Wishing all my Muslim Brothers and Sisters a fruitful RAMADAN, may Allah forgive all our sins and accept our fast.
.