Monday, July 29, 2013

Mbaazi za kupaka

Mahitaji
ü  Mbaazi mbichi au Mbaazi kavu - ½ kl                           
ü  Kitunguu maji - Kikubwa kimoja 1
ü  Kitunguu swaum – Kiasi cha punje nne/tano
ü  Karoti – Moja kubwa
ü  Pili pili hoho – Moja kubwa
ü  Chumvi - Kiasi
ü  Manjano - ½ Kijiko cha chai
ü  Mafuta ya kupikia (Vegetable oil) – Kijiko kimoja  cha chai
ü  Pilipili mbichi – Moja moja nzima
ü  Nazi (Coconut nature) – Tatu kubwa 
ü  Giligilan
ü  Unga wa ngano (Plain flour) – kijiko kimoja cha chakula

Matayarisho na kupika
Hatua ya kwanza:
ü  Osha mbaazi kwenye chungio na ziache zitoke maji.
ü  Chambua kitunguu maji chako, kisafishe na ukikate vipande vidogo vidogo katika shape nzuri .
ü  Chambua kitunguu swaum vyako vitwange mpaka vilainike vizuri.
ü  Osha karoti na pili pili hoho kisha uvikate vidogo vidogo katika shape nzuri
ü  Kuna nazi (coconut nature) yako vizuri iwe laini na uichuje matui mawili, tui bubu(tui la kwanza) na tui la pili.

Kupika kwa mbaazi mbichi
ü  Chemsha mbaazi zako mbichi kwa maji hadi ziive lakini zisirojeke ziwe ngumu kidogo.
ü  Chukua tui lako la weka kwenye mbaazi zako pamoja na mchanganyiko wa karoti na nk.
ü  Weka tena jikoni vichemke na mpaka tui lako likauke kabisa.
ü  Mimina mbaazi zako kwenye trei ili zipoe na ni vyema zikapoa kabisa ili tui lako ukija kumwagia juu lisiyeyuke.
ü  Chukua tui lako bubu weka jikoni, weka kijiko cha chakula plat unga wa ngano (Plain flour).
ü  Koroga bila ya kuacha hadi tui lako lichemke, kisha koroga manjano yako kwenye kikombe weka kiasi.
ü  Changanya kwenye tui lako unalo lipika akikisha tui lako lina kua zito zito.
ü  Ipua na pooza kodogo tui lako.
ü  Mwagia juu ya mbaazi ukiwa unasambaza kama icesugar kwenye cake.

Kupika kwa mbaazi kavu
ü  Chambua mbaazi na kutoa uchafu osha na loweka mbaai zako usiku kucha.
ü  Mbaazi zina tabia ya kunyonya maji hivyo basi weka kwenye kikubwa na ujaze maji
ü  Asubuhi zitoe kwenye maji na ubadike jikoni weka maji hadi zitakapo anza kuiva
ü  Punguza moto ili ziive kwa moto mdogo ili zisi pasuke.
ü  Chuja nazi na tui bubu weka pembeni tumia lile tui la pili.
ü  Hilo tui la pili weka kwenye mbaazi zako pamoja na mchanganyiko wako wa vitunguu maji, hoho na nk.
ü  Weka tena jikoni ili hilo tui la pili na mchanganyiko wako uchanganyike na tui lako liivi na likauke.
ü  Ipua na umimine kwenye trei wacha zipoe.
ü  Chukua tui lako bubu weka jikoni, weka kijiko cha chakula plat unga wa ngano (Plain flour).
ü  Koroga bila ya kuacha hadi tui lako lichemke, kisha koroga manjano yako kwenye kikombe weka kiasi.
ü  Changanya kwenye tui lako unalo lipika akikisha tui lako lina kua zito zito.
ü  Ipua na pooza kodogo tui lako.
ü  Mwagia juu ya mbaazi ukiwa unasambaza kama icesugar kwenye cake.
ü  Na baada aya hapo mbaazi zako zitakua tayari kwa kuliwa

Kumbuka:
kuanza maandalizi mapema ili tui ligande kwenye mbaazi zako.
Unaweza kulia na chochote kile, iwe chapati, wali, maamri (maandazi),vitumbua yani raha tupu.

Pishi:
Limetetwa kwenu na bidada Sware Kaku. Asante sana mama naenda fanyia kazi hii kitu.
Ramadan kareem na siku njema kwetu sote In Sha Allaah. 

Thursday, July 25, 2013

Tahadhari

Amyna naamini ni mzima wa afya na unaendelea vyema na mfungo mtukufu wa ramadhan.
Tafadhali publish ujumbe huu ili kila mtu awe na tahadhali na wizi ulio ibuka sasa na unaendelea kwa kwasi hapa jijini
 
Kuna taarifa ya utapeli hatari umeingia mjini watu wanajifanya wanauza manukato (Perfumes).
Watakushawishi unuse kipande cha karatasi ambacho kimenyunyuziwa dawa yenye sumu – wao watakwambia Perfumes wanayo taka kukuuzia ndio wamepulizia hapo wwe utaamini na kunusa ili usikilize harufu yake kumbe sio manukata hayo ni kitu ningine ambayo ukinusa  tu unaweza kujikuta umepoteza fahamu na hapo unawapa nafasi ya kukuibia ulicho nacho.
Tafadhari kuwa mwangalifu unapokutana na watu kama hao. Tafadhali wafahamishe ndugu, jamaa na rafiki habari hii na wote tuwe makini pindi unapo kutana na kitu kama hicho.

Asante Fatma ujumbe nimeupata na ndio huo nimeufanyia kazi.
Ramadan Kareem na Siku Njema.

Monday, July 22, 2013

Chapati

Wadau Asalaam Aleykum kwa Waislam wote na Bwana Asifiwe kwa Wakristu wote.
Leo dada yenu naja na pishi la CHAPATI. Najua ni kitafundwa pendwa sana na kinapendwa na kila lika.
Uzuri wake chapati bwana unaweza kulia na chochote kile, iwe maharage, supu aina zote, mchuzi uwe wa kuku, wa samaki, wa nyama yani raha tupu hapa hata na chai inapanda kwa soda na juice tena ndio balaaa.
Kwa kipindi hiki cha mfungo mtukufu wa Ramadan chapati hua zinalika hasa tena sana sana hua zinaambatana na mchuzi no matter wa kitoweleo gani.
Tuungane pamoja katika safu yetu na tushare pamoja mawazo yetu.
 
 
Mahitaji
ü  Unga wa ngano (Plain flour 1kilo)
ü  Siagi (Butter vijiko 2 vya chakula)
ü  Yai (Egg 1)
ü  Chumvi (1/2 ya kijiko cha chai)
ü  Hiliki (Ground cardamon 1/4 ya kijiko cha chai)
ü  Maji ya uvuguvugu (Warm water)
ü  Mafuta ya kupikia (Vegetable oil)
 
Matayarisho
Weka unga wa ngano katika bakuli la kukandia, kisha tia chumvi na  hiliki iliyo twangwa na uchanganye kwanza mpaka mchanganyiko wako uchanganyike.
Tia siagi na uichanganye vizuri na unga mpaka ipotee. Baada ya hapo tia tena yai na uchanganye vizuri.
Mchanganyiko ukishachanganyika vizuri sasa unaweza kutia maji ya uvuguvugu kidogo, kidogo huku ukiwa unauchanganya ili kupata donge.

Baada ya hapo anza kukanda hilo donge mpaka mabuje yote yapotee na unga uwe laini.
ambapo itakuchukua kama dakika kumi au kumi na tano hivi. Baada ya hapo kata kata unga wako katika madonge ya wastani yani si makubwa si madogo.
Baada ya hapo andaa kibao cha kusukumia chapati kwa kukitia unga kidogo ili chapati isinatie kwenye kibao.
Sukuma donge moja la chapati mpaka liwe flat na kisha weka kijiko kimoja cha mafuta na usambaze.
Ukisha maliza ikunje (roll). Ufanye hivyo na kwa madonge yote yalio bakia.
Baada ya hapo andaa chuma cha kuchomea (fry-pan) katika moto wa wastani.
Kisha anza kusukuma chapati (ni vizuri ukaanza na zile ulizozikunja mwanzo ili kuzipa nafasi zile za mwisho ziweze kulainika).
Ukiwa unasukuma hakikisha zinakuwa flat (na zisiwe nene sana au nyembamba sana) Ukishamaliza hapo tia kwenye chuma cha kuchomea.
Acha iive upande mmoja kwanza alafu uigeuze na  upande wa pili.
Tia mafuta ama kijiko kimoja kikubwa upande wa chini wa chapati na uanze kuukandamiza kwa juu uku ukiwa unaizungusha.
Utaendelea kufanya hivyo uku ukiwa unaigeuza kuiangalia kwa chini ili isiungue. ikishakuwa ya brown, geuza upande wa pili na urudie hivyo hiyvo mpaka chapati iive.
Utaitoa na kuiweka kwenye sahani na itakua tayari kwa kuliwa.

Utafanya hivyo kwa madonge yako ya chapati yote yaliyo bakia.

Swaum Njema na Ramadan Kareem.

Tuesday, July 16, 2013

Take It or Leave It

Facts of Life
Important
May Allah forgive us our sins and  accept our prayers, bless us with his love and care, throught out life and hereafter.

Wishing you a wonderful Ramadan.

Friday, July 12, 2013

Hijab styles

It’s all about swagzzz…. Hahahaha ona swag za hijab hadi za watoto
 

 Open hii link ku-enjoy zaidi 
 
Swaum njema.
Ramadan Maqbul & Jumaa Mubarak

Thursday, July 11, 2013

Ramadan Kareem

It’s officially RAMADAN Alhamdulillah.
 
May Allah keep us steadfast on the Deen and may he make this month a means to grant us Jannah.
 
Note: When the month RAMADAN start the gates of the heaven are opened and the gates of hell are closed, also the devils are chained.
 
 
 
Wishing all my Muslim Brothers and Sisters a fruitful RAMADAN, may Allah forgive all our sins and accept our fast.
.