Tuesday, April 08, 2014

Mambo nane yakuyajua kuusu wanawake

http://www.baumorthodonticaligners.com/images/start.jpg

Mtu Mmoja mwenye hekima alisema: "Jihadhari na kuwadanganya wanawake kwani wana uhodari wa kujua ukweli na uwezo mkubwa wa kujifanya hawajui". Mwenye kupoteza penzi la mwanamke mwaminifu, amepoteza maisha yake yote.

 
 Je unajua kwamba:-
  1. Mwanamke akiwasiliana nawe sana anamaanisha hataki kuongea na mwingine.
  2. Mwanamke aliyeachwa mara nyingi hupata mwanamme bora kwasababu amejifunza kuchagua kutokana na jeraha lake.
  3. Mwanamke anamiliki hisia sita zaidi ya mwanamme anajua akibadilika au akimsaliti.
  4. Mwanamke anasubiri na kuvumilia sana kuliko mwanamume.
  5. Mara nyingi mwanamke akinung'unika anapendelea kunyamaza.
  6. Mwanamke anaporeact na kukulaumu kwa kosa ambalo wewe ungemtukana, kumpiga au hata kumuacha anamaanisha anakupenda sana.
  7. Mwanamke anapokua amekerwa na mwanamme akanyamaza anatarajia kuwa atabadilika na sio kwa kutojua.
  8. Mwanamke akizungumziwa na mwanamme kuhusu mwanamke mwingine, huficha kilio chake nyuma ya tabasamu lake. 
Kivyo basi usione anacheka unavyowasifia wanawake wengine.
Embu tujuzane wadau kuna ukweli kwenye hili? Mimi naona kama upo vile.


5 comments:

  1. Mweeeee kweli tupu

    ReplyDelete
  2. almost point zote hizo zina ukweli. yani umemgusa mwanamke hasa hasa

    ReplyDelete
  3. Huyu ndio mwanamke bana

    ReplyDelete
  4. Wanawake bana wanavitu vingi sana vya kimya kimya na usipo kua nao makini utakua njia panda kila uchao.

    ReplyDelete