Showing posts with label Mapishi. Show all posts
Showing posts with label Mapishi. Show all posts

Friday, July 11, 2014

Mapishi ya Kebabu

Haya jongeeni kijiweni tuongezeane ujuzi wa mapishi. Angalia upishi wa KEBABU.
Mahitaji
 1. Nyama ya kusaga kl 1
 2. Kotmili/giligilani wengine huita kifungu kimoja
 3. Kitunguu maji vikubwa vitatu
 4. Swaum kikubwa kimoja & tangawizi
 5. Mikate ile ya elfu moja nunua miwili ama mitatu
 6. Chumvi kiasi
 7. Binzali nyembamba na pilipili manga vilivyo sagwa
 8. Pili pili hoho kubwa moja
 9. Mafuta ya kupikia
 10. Ndimu
 11. Mayai sita
Hatua ya kwanza
Nyama ya kababu hua aichemshwi habisa. Kumbuka nyama kama ina maji yakamua. Chukua nyama yako weka kwenye chombo kisafi, tia chumvi, ndimu, unga wa binzari nyembamba, kamulia na ndimu kisha tia pilipili manga, alafu changanya huo mchanganyiko wako na uakikiche umechanganyika vizuri kabisa.
Hatua ya pili
Katakata vitunguu maji katika vipande vidogo vidogo kama vya sambusa vile, katakata pia pili pili hoho zako katika mfumo huo huo pamoja na karoti, osha kotmili/giligilani zako vizuri na ukamue maji alafu toa ile mizizi ya nyuma na kisha katakata katika vipande vidogo vidogo, twanga swaum zako pamoja na tangawizi na badala ya hapo tia katika mchanganyiko wako ule wa nyama. Changanya mpaka uakikiche umechanganyika vizuri. Kuonja ruksa wapenzi iliuweze jua kama vitu vyote vipo sawa au laa....
Hatua ya tatu
Chukua mikate yako toa ile nyama ya kati nikimaanisha ile nyama ya mkate nyeupe ule upindo wa pembeni usiweke sababu ni mgumu na sio soft. Chambua mikate yako vizuri kabisa na inyambue nyambue na uweke katika mchanganyiko wako wa nyama, chukua mayai matatu uweke humo. Changanya vyote sasa kwa pamoja mpaka uwakikiche vimechanganyika ipasavyo. Na baada ya hapo utafanya kama unakanda unga wa ngano vilee na upate donge moja takatifu. Utaacha mchanganyiko wako kwa mda wa kama dk 10 or 15 hivi ili viungo viweze kukolea kwa uzuri.
Hatua ya nne na mwisho
Kata vidonge vidodo vidogo ama upendavyo na kutengeneza style uipendayo, weka kwenye chombo safi, vyunja mayainyako yale matatu yalio baki na uweke kwenye bakuli toa vile viini vya ndani na ubaki na ute tu. Weka kikaangio chako jikoni na usiwe na moto mkali, moto uwe wa wastani tu, mafuta yako yakisha pata moto chukua kebabu zako tosa kwenye ule ute wa yai na uweke kwenye mafuta yakio jikoni na utarudia kwa vyote viduara ulivyo fanya. Baada ya hapo vitakua tayari kwa kuliwa. Ni tamuje sasa.....Very yummy waweza sukumia na chochote Wallah.

Cha ziada
Wapenzi alafu ule mkate ulio utoa ule mgumu (upindo wa mkate) hautupwi wapendwa. Unaufanya hivi; Ukaushe kwenye microwave ukauke vizuri usiungue. Alafu utwange huo mkate wako mpaka upate unga unga. Baada ya kukata madonge yako ya kebabu unaweka kwenye huo unga viliga viliga ukitoa unaweka kwenye ute wa yai utafanya hivyo mara mbili na kasha utachoma.









Amynag tunawapenda sana 
Ramadan Makbul & Ijumaa Kareem.
Enjoy


Monday, July 22, 2013

Chapati

Wadau Asalaam Aleykum kwa Waislam wote na Bwana Asifiwe kwa Wakristu wote.
Leo dada yenu naja na pishi la CHAPATI. Najua ni kitafundwa pendwa sana na kinapendwa na kila lika.
Uzuri wake chapati bwana unaweza kulia na chochote kile, iwe maharage, supu aina zote, mchuzi uwe wa kuku, wa samaki, wa nyama yani raha tupu hapa hata na chai inapanda kwa soda na juice tena ndio balaaa.
Kwa kipindi hiki cha mfungo mtukufu wa Ramadan chapati hua zinalika hasa tena sana sana hua zinaambatana na mchuzi no matter wa kitoweleo gani.
Tuungane pamoja katika safu yetu na tushare pamoja mawazo yetu.
 
 
Mahitaji
ü  Unga wa ngano (Plain flour 1kilo)
ü  Siagi (Butter vijiko 2 vya chakula)
ü  Yai (Egg 1)
ü  Chumvi (1/2 ya kijiko cha chai)
ü  Hiliki (Ground cardamon 1/4 ya kijiko cha chai)
ü  Maji ya uvuguvugu (Warm water)
ü  Mafuta ya kupikia (Vegetable oil)
 
Matayarisho
Weka unga wa ngano katika bakuli la kukandia, kisha tia chumvi na  hiliki iliyo twangwa na uchanganye kwanza mpaka mchanganyiko wako uchanganyike.
Tia siagi na uichanganye vizuri na unga mpaka ipotee. Baada ya hapo tia tena yai na uchanganye vizuri.
Mchanganyiko ukishachanganyika vizuri sasa unaweza kutia maji ya uvuguvugu kidogo, kidogo huku ukiwa unauchanganya ili kupata donge.

Baada ya hapo anza kukanda hilo donge mpaka mabuje yote yapotee na unga uwe laini.
ambapo itakuchukua kama dakika kumi au kumi na tano hivi. Baada ya hapo kata kata unga wako katika madonge ya wastani yani si makubwa si madogo.
Baada ya hapo andaa kibao cha kusukumia chapati kwa kukitia unga kidogo ili chapati isinatie kwenye kibao.
Sukuma donge moja la chapati mpaka liwe flat na kisha weka kijiko kimoja cha mafuta na usambaze.
Ukisha maliza ikunje (roll). Ufanye hivyo na kwa madonge yote yalio bakia.
Baada ya hapo andaa chuma cha kuchomea (fry-pan) katika moto wa wastani.
Kisha anza kusukuma chapati (ni vizuri ukaanza na zile ulizozikunja mwanzo ili kuzipa nafasi zile za mwisho ziweze kulainika).
Ukiwa unasukuma hakikisha zinakuwa flat (na zisiwe nene sana au nyembamba sana) Ukishamaliza hapo tia kwenye chuma cha kuchomea.
Acha iive upande mmoja kwanza alafu uigeuze na  upande wa pili.
Tia mafuta ama kijiko kimoja kikubwa upande wa chini wa chapati na uanze kuukandamiza kwa juu uku ukiwa unaizungusha.
Utaendelea kufanya hivyo uku ukiwa unaigeuza kuiangalia kwa chini ili isiungue. ikishakuwa ya brown, geuza upande wa pili na urudie hivyo hiyvo mpaka chapati iive.
Utaitoa na kuiweka kwenye sahani na itakua tayari kwa kuliwa.

Utafanya hivyo kwa madonge yako ya chapati yote yaliyo bakia.

Swaum Njema na Ramadan Kareem.

Friday, August 03, 2012

Kachori

Maitaji ya pishi la kachori
o   Viazi (mbatata) vikubwa kiasi 5
o   Thomu na Tangawizi Kijiko 1 cha chakula
o   Chumvi Kijiko 1 cha chai
o   Pilipili ya kusaga kutegemea na unavyoipenda
o   Ndimu 1
o   Pilipili mboga (Pili pili hoho) 1
o   Karoti 1
o   Mafuta ya kupikia
o   Unga wa dengu au Ngano Kiasi

Namna ya kutayarisha na kupika
o   Chemsha viazi mpaka viwive, kisha vitoe maganda na uviweka ndani ya bakuli.
o   Sukua karoti yako na mashine zile za mkono au unaweza kukata kata vipande vidogo vidogo, pia kata kata karoti yako vipande vidogo vidogo na uvichemshe kwa dakika moja au mbili tu.
o   Tia katika chombo viazi mbataba vyako na uviponde ponde mpaka viwe laini usiongeze maji. Unaweza tumia mwiko kusaga viazi nyako.
o   Saga thomu na tangawizi kisha changanya na viazi.
o   Weka chumvi, ndimu na pilipili ya unga kisha uonje, unaweza kuongeza viungo kwa jinsi upendavyo.
o   Tengeneza magonge ya duara yenye ukubwa kiasi au unaweza tengeneza style yoyote upendayo na uyaweke kwenye sahani.
o   Chukua unga wako wa ngano au unga wa dengu utie kwenye bakuli na unganganye na maji, ujiji huu usiwe mzito sana na wala usiwe mwepesi sana unapendeza ukiwa size ya kati.
o   Bandika mafuta yako ya kula jikoni yakiwa kwenye karai na subili mafuta yapate moto.
o   Kuchua madonge yako uliyo yaandaa na ujatose kwenye uji uji wako wa ngano au uji uji wa dengu alfu toa na uyatie kwenye karai la mafuta subilia zichomeke na kubadilika rangi kidogo.
o   Toa kachori zako weka pembeni zijichuje mafuta na zipange vizuri kwenye sahani na zitakua tayari kwa kuliwa.


Dokezo:
 Kachori inaliwa wakati wowote na mtu yoyote pia sio lazima utie pili pili kama wewe sio mpenzi wa pili pili ni kitafunwa kizuri sana kwa kweli, kwanza soft hakiitaji nguvu wakati unakula.

Nawapenda sana na nawatakia Ramadhan Kareem.