Thursday, January 30, 2014
Friday, January 24, 2014
Namna ya kupunguza unene ndani ya siku saba
Siku
ya 1:
Asubuhi kula matunda (lakini usile ndizi). Mchana chemsha kabichi, weka chumvi
kidogo na nyanya, chemsha na upate supu. Kula mchanganyiko huo na utajiona
umeshiba. Jioni kula tikiti maji na mbogamboga au kabichi uliyotengeneza
mchana.
Siku
ya 2:
Kula mboga za majani asubuhi (usile mboga za majani zenye wanga kama karoti).
Mchana kula kabichi iliyochemshwa, tengeneza na kachumbari. Katika kabichi weka
chumvi, pilipili na mafuta ya olive. Jioni unaweza kula mlo kama wa mchana
lakini unaweza kukaanga mboga nyingine za majani.
Siku
ya 3: Kula mboga za majani na matunda, unaweza kuongeza
kiazi kitamu kimoja.
Siku
ya 4: Kula ndizi moja na unywe na maziwa ya mtindi
wakati wa asubuhi. Mchana kula kabichi kama ulivyoitengeneza kwenye siku ya
kwanza, usiku rudia mlo wa mchana.
Siku
ya 5: Kula nyanya nne pamoja na samaki au kipande cha
kuku asubuhi. Mchana unaweza kula samaki wa kuchemsha kiasi ambaye
amechanganywa na nyanya. Wakati wa jioni unaweza kula chakula kama cha mchana.
Siku
ya 6: Unaweza kula chakula cha protini na mboga za
majani. Anza kwa kula kachumbari asubuhi. Mchana kula tambi kiasi na kipande
kidogo cha samaki. Usiku tengeneza supu ya kabichi.
Siku
ya 7: Anza kwa matunda na juisi. Mchana kula mboga za
majani na usiku kula supu ya kabichi na kiazi kimoja.
Kumbuka:
Unatakiwa kunywa maji kwa wingi. Usiendelee kwa muda mrefu.
TeamDiet
mpooo hapo. Hii kitu nimetumiwa na rafiki yangu Jully nikaona sio mbaya nishare
nanyi vipenzi nyangu sababu najua wanene tupo wengi hasaa na tunataka sana
kupungua. Diet hii niya mboga mboga na matunda.TeamDiet haya twende kazi.
Jully
my dear much respect mama.
Monday, January 20, 2014
Mabadiliko baraza la mawaziri Tanzania
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete amefanya mabadiliko katika baraza lake la mawaziri kwa kuwateua
mawaziri na manaibu waziri, kuziba nafasi zilizoachwa na mawaziri wanne
waliojiuzulu na mmoja aliyefariki dunia hivi karibuni. Katika
uteuzi huo Rais Kikwete amewateua mawaziri wapya wawili na manaibu waziri wapya
wanane, huku akiwapandisha vyeo manaibu waziri wanne kuwa mawaziri kamili. Miongoni
mwa mawaziri wapya ni pamoja na aliyewahi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa
Mataifa, Dokta Asha-rose Migiro, ambaye ameteuliwa kuwa waziri wa Katiba na
Sheria, huku Dk. Titus Kamani akiteuliwa kuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na
Uvuvi.
Waziri pekee aliyeachwa katika
mabadiliko hayo ni aliyekuwa waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais,
(Mazingira), Dk. Terezya Huvisa. Miongoni mwa manaibu waziri wapya ni pamoja na
Juma Nkamia ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari na mtangazaji, ambaye
amepewa dhamana katika Wizara ya Habari, Vijana na Michezo.
Mabadiliko yaliyofanywa na Rais
Kikwete yametokana na kujaza nafasi za mawaziri ambao walilazimika kujiuzulu
baada ya ripoti ya bunge kuhusu Operesheni Tokomeza Ujangili kubaini kuwepo
vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na mauaji, utesaji
na udhalilishaji vikidaiwa kutendwa na watekelezaji wa operesheni hiyo.
Ripoti hiyo iliwalazimisha
waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki kutangaza kujiuzulu,
huku naye waziri wa mambo ya ndani, Dr. Emmanuel Nchimbi kufuata mkondo huo
bila kumwaacha waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa, Shamsi Vuai Nahodha,
na Dr. Mathayo David Mathayo aliyekuwa waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi,
kutokana na wizara zao kuhusika katika usimamizi wa operesheni hiyo ambayo
iliwahusisha polisi, askari jeshi na walizni wa wanyamapori. Huku nafasi ya
tano katika baraza hilo ikiachwa wazi na aliyekuwa waziri wa fedha, Dr. William
Mgimwa aliyefariki dunia mapema mwezi huu nchini Afrika Kusini alikokuwa
akipata matibabu.
Subscribe to:
Posts (Atom)





